Monday 4 May 2015

Patcho Mwamba: Hamna star wa kike ana nyota kama ya Wema Sepetu, ila dhambi yake ni moja...

 
Mwanamuziki wa band ya Fm Academia Patcho Mwamba ambae pia ni muigizaji wa filamu, amejibu swali aliloulizwa kwenye mahojiano maalumu na Bestizzo "Je unahisi Wema halitendei haki jina lake au kuna sehemu anakosea?"

''Kwanza tuseme ukweli wa Mungu hamna star wa kike ana nyota kama ya Wema Sepetu, ni star ni star ni star ni star sana upande wa wanawake wote ndani ya bongo ila dhambi yake moja ni kuanika sana maisha yake... akiwa na mpenzi jamani mpenzi wangu ndio huyu hapa akiachana nae ni rahisi watu kujua...''

Monday 27 April 2015

Ommy Dimpoz Aikana 'KICK' ya Wema Sepetu ,Adai Hawezi kuwa Mapenzini na Wema Kwasababu Anaweza Kuharibu Mambo yake ya Maana


Msanii mkubwa Bongo Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz amesema kuwa hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu kwa sababu anaweza kuharibu mambo yote ya maana ambayo anapanga kuyafanya.
Dimpoz aliweka wazi hayo kwa Dia wa ala za Roho na kusema kuwa Wema ni staa na ni mzuri hana tatizo lakini mazingira yanachangia awe mbali nae kwani akiweka mapenzi kutakuwa hakuna kazi.

"Unajua ukiwa na rafiki alafu mkaweka mapenzi basi patakuwa hakuna kazi zaidi ya kuharibu kazi , hata kama palikuwa na project basi mwishowe inaharibika, Nasisitiza sina uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu" Alisema Dimpoz